Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Maji

Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria

LVBWB yatambua mchango wa Mhandisi Jane Mrosso

Imewekwa: 07 August, 2026
LVBWB yatambua mchango wa Mhandisi Jane Mrosso

Kwa utambuzi wa mchango wake mkubwa, kujitoa na ustahimilivu,uadilifu na kujituma katika utumishi wa umma, Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria kupitia Mkurugenzi wake, Dkt. Renatus Shinhu, imemtunuku
Meneja wa Mazingira na Uratibu wa Jumuiya za Watumia Maji, Mhandisi Jane Mrosso, tuzo maalum ya
"Tenacity and Commitment".
Tuzo hiyo, ikiambatana na cheti cha utambuzi, ilitolewa katika hafla fupi ya kuwaaga waliokuwa
watumishi wa Bodi hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuthamini utendaji bora, ustahimilivu, uaminifu na kujitolea kwa watumishi
wanaotoa mchango chanya katika kufanikisha majukumu ya taasisi.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mhandisi
Jane Mrosso alishukuru Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria kwa kutambua mchango wake na kusema kuwa tuzo hiyo ni heshima kubwa sana kwake ambayo hakutegemea kuipata.
Alisema heshima hiyo imetokana utendaji kazi, uwajibikaji na ushishirikiano wa team kubwa ya watumishi wa Bodi na kuwahimiza watumishi wenzake kuendelea kutumikia umma kwa moyo wa kujituma.
Kwa upande wake, Dkt. Renatus Shinhu alisema tuzo ya "Tenacity and Commitment" inalenga kuhamasisha utamaduni wa uwajibikaji, uadilifu na ubora wa
utendaji kazini. Alibainisha kuwa Mhandisi Mrosso ameonesha mfano wa kuigwa katika utekelezaji wa
majukumu yake na kwamba utambuzi huo uwe chachu kwa watumishi wengine ndani na nje ya taasisi kuendelea kutekeleza wajibu wao kwa uaminifu,
weledi na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma.