BODI YA MAJI BONDE LA ZIWA VICTORIA YATOA MAFUNZO YA AFYA YA AKILI KWA WATUMISHI WAKE
Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria, kwa kushirikiana na Hospitali ya
Rufaa ya Kanda ya Bugando, imeendesha mafunzo ya afya ya akili kwa
watumishi wake ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ustawi wa afya na
kuongeza tija mahali pa kazi.
Mafunzo hayo yaliyowakutanisha
watumishi kutoka madakio yote ya Bodi, yamefanyika katika Ofisi Kuu ya
Bodi iliyopo jijini Mwanza.
Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi wa
Bodi, Dkt. Renatus Shinhu, amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya
utekelezaji wa mpango wa Serikali na Bodi wa kuimarisha ustawi wa
watumishi kwa kuwajengea uwezo wa kutambua, kuzuia na kukabiliana na
changamoto za afya ya akili ili waendelee kutekeleza majukumu yao kwa
ufanisi, utulivu na weledi.
Baada ya mafunzo, watumishi walifanya
kikao cha robo mwaka ambapo walijadili masuala mbalimbali ya
kiutumishi, kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za Bodi pamoja na
taarifa za matumizi na masuala mengine muhimu yanayohusu maendeleo ya
taasisi.
Mikutano hiyo ya robo mwaka imeendelea kuwa sehemu ya
utamaduni wa Bodi wa kuimarisha mawasiliano ya ndani, ushirikiano
miongoni mwa watumishi na ustawi wao, sambamba na kuhakikisha mazingira
bora ya kazi kwa ajili ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi.