Bodi ya maji Bonde la Ziwa Victoria leo Oktoba 11, 2022 imepokea ugeni wa maafisa wa kijeshi kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha Duluti Arusha kwa ajili ya ziara ya kujifunza shughuli za bodi katika usimamizi wa rasilimali za maji ndani ya bonde.Maasifa hao wakiongozwa na Brigedia Jenerali Sylvester Ghuliku ni kutoka Tanzania, Rwanda, Misri, Burundi, Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo, Uganda, Nigeria, Malawi, na Kenya, na wamepokelewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria, Bwana Renatus Shinhu.Brigedia Jenerali Sylvester Ghuliku alisema lengo la ziara ya maofisa hao ni kujifunza shughuli za usimamizi wa rasilimali maji ikiwa ndio kiungo kikubwa cha kiuchumi hasa Ziwa Victoria linalotegemewa na nchi nyingi barani Afrika kwa shughuli za kimaendeleo.Kwa upande […]
Kategorie: Uncategorized
UZINDUZI WA MIRADI YA UHIFADHI WA VYANZO VYA MAJI ZANZUI NA MWADILA
Waziri wa Maji, Mheshimiwa Jumaa Aweso Julai 29, 2022 amezindua miradi miwili ya uhifadhi wa vyanzo vya maji vya Zanzui (New Sola ) na Mwadila vilivyopo Wilaya ya Maswa. Katika uzinduzi huo Mheshimiwa Aweso aliipongeza Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria kwa kazi kubwa waliyofanya ya kuhifadhi vyanzo hivyo kwa kishirikiana na viongozi wa Wilaya na jamii. “Usimamizi wa vyanzo vya maji ni shirikishi na hapa Zanzui na Mwadila mmeweza, inawapongeza sana,” alisema Waziri Aweso. Awali, akitoa taarifa ya miradi hiyo, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria, Bwana Renatus Shinhu alisema tayari Bodi imeweka mipaka ya kudumu katika chanzo cha Zanzui na wamesimika vigingi 250 kuzunguka eneo la chanzo hicho, pia kumepandwa miti 20,000. Mambo mengine […]
MKUTANO WA SEKTA NYINGI ZA BONDE
Mkutano wa sekta nyingi wa bonde. Misingi ya mkutano Mkutano wa sekta nyingi hufanyika kipindi ambacho Tanzania kama nchi imepata uzoefu wa Zaidi ya robo karne kuhusu jinsi ya kusimamia vyanzo vyake vya maji ikiongozwa na kanuni za IWRM. Mipaka ya kihaidrolojia ikiwa kama vipimo vya makadirio, nchi nzima iligawanywa katika mabonde tisa ya mito na maziwa ikiwemo bodi ya maji bonde la ziwa Victoria iliyoanzishwa mnamo mwaka 2000 chini ya sheria ya matumizi ya maji (udhibiti na taratibu) nambari 42 ya mwaka 1974 iliyotenguliwa na nafasi yake kujazwa na sheria ya usimamizi wa rasilimali maji nambari 11 ya mwaka 2009. Mkutano huu ni ari katika kuanzisha njia rasmi na yenye nguvu katika kuwahusisha washikadau mbalimbali katika wingi wao na […]